• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kampuni ya China ya Hengya Cement yawekeza Tanga,kutoa ajira 5,000 kwa vijana

    (GMT+08:00) 2018-11-05 19:39:17

    Kampuni ya Hengya Cement Company Ltd ya China imewekeza ujenzi wa viwanda 11 katika eneo la kijiji cha Mtimbwani wilayani Mkinga mkoani Tanga ambapo vijana zaidi ya 5,000 watapata ajira.

    Hayo yalibainishwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella,kwa Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa ,alipotembelea eneo la ujenzi na kuweka saini ya uzinduzi wa ujenzi huo wa viwanda 11.

    Alisema kati ya viwanda hivyo 11 kipo kiwanda kikubwa cha kutengeneza saruji ambacho kitakuwa cha kwanza kwa ukubwa Afrika Mashariki na kuzalisha tani milioni saba kwa mwaka na ajira takriban 5,000.

    Shigella alisema wawekezaji hao kutoka China wamechagua kuwekeza viwanda hivyo katika kijiji cha Mtimbwani kwa kuwa kuna mazingira mazuri.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako