Katika notisi ambayo KRA ilitumia walipa ushuru wiki mbili zilizopita,ilitoa onyoa kwa waliokwepa kulipa ushuru kufanya hivyo kabla ya makataa ya tarehe 9 Novemba au kuchukuliwa hatua zaidi.
Licha ya notisi hizo kutolewa,walipa ushuru wengine wamelalama wakisema kuwa wametumiwa notisi hizo kimakosa kwani wao wameshalipa ushuru na hawana deni lolote na Mamlaka ya Mapato.
Hata hivyo KRA imesema notisi hizo ni za mfumo wa kielektroniki kwa muda ambao walipa kodi walikosa kulipa kwa wakati uliowekwa kisheria.
KRA hivi karibuni ilianzisha mfumo mpya ambao unawatambua walipa kodi,madeni,faini na riba,ambapo baadae maafisa wanapewa majukumu ya kufuatilia na kuhakikisha madeni yanalipwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |