Haya yalithibitishwa na Meneja wa CRDB tawi la Kibaha, Rosemary Nchimbi, alipokuwa akizungumza na viongozi mbalimbali wa Serikali, wakiwamo Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, Waziri wa Nishati. Dk. Medard Kalemani na wananchi mbalimbali waliokuwa wametembelea maonyesho hayo.
Nchimbi, alisema kuwa, CRDB iliamua kuwadhamini wajasiriamali hao ili waweze kupata fursa ya kushiriki maonyesho hayo na kutangaza bidhaa zinazotengenezwa kupitia vikundi vyao.
Pamoja na hayo, Nchimbi aliwataka wajasiriamali ambao wapo nje ya vikundi, kuhakikisha wanajiunga kwa haraka kwenye vikundi ili waweze kufaidika na fursa za mikopo na pamoja na udhamini mwingine unaotolewa na CRDB.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |