• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jonesia kuchezesha Afcon ya wanawake Ghana

    (GMT+08:00) 2018-11-06 09:50:42

    Mwamuzi wa Tanzania, Jonesia Rukyaa, amechaguliwa kuchezesha fainali za Afrika za wanawake zitakazofanyika nchini Ghana mwaka huu. Jonesia amechaguliwa katika orodha ya waamuzi wa katikati akiwa ni Mtanzania pekee katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Novemba 17 hadi Desemba 1, mwaka huu.

    Akizungumza Dar es Salaam, Ofisa habari wa shirikisho la soka Tanzania (TFF), Clifford Ndimbo, amesema Rukyaa amechaguliwa katika orodha ya waamuzi 13 wa katikati na wasaidizi 12.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako