Rais Xi Jinping wa China ametuma barua ya pongezi kwa Mkutano wa 5 wa Dunia kuhusu Mtandao wa Internet ulioanza hii leo mjini Wuzhen, mkoa wa Zhejiang, mashariki mwa China.
Katika barua hiyo, rais Xi amesema inapaswa kuongeza kasi ya maendeleo ya uchumi wa kidijitali na kuboresha mfumo wa usimamizi wa mtandao wa internet duniani ili uendelee kwa njia sahihi na inayoeleweka. Amesema licha ya kuwa na mazingira tofauti na kukabiliwa na changamoto mbalimbali, nchi zote duniani zina haja sawa ya kuboresha uchumi wa kidijitali, maslahi katika kushughulika na changamoto zinazotokana na usalama wa mtandao wa internet, na mahitaji ya usimamizi bora wa mtandao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |