Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo,Kamimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB,Japhet Justine,amesema TADB inalenga kuwawezessha wakulima wa zao la pamba nchini Tanzania ili kuongeza tija na uzalishaji kama inavyobainishwa katika Mpango wa Maendeleo ya kilimo Awamu ya Pili (ASDP-11).
Alisema matrekta ni sehemu ya utekelezaji wa ASDP-11 katika kuhakikisha nyenzo bora za kilimo zinawafikia wakulima na kuchagiza uzalishaji zaidi wa malighafi zitakazotumika kwenye viwanda na kufanikisha azma ya serikali ya kujenga uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2025.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |