Hii ni sehemu ya 'Wiki ya Wajasiriamali Ulimwenguni' ambayo itawaleta pamoja wajasiriamali zaidi ya 4,000 haswa vijana na wanawake,kujadiliana jinsi watakavyoweza kuboresha biashara zao.
Pia inalenga kujadili changamoto zinazowaathiri wajasiriamali wanawake ,upatikanaji wa fedha ,miongoni mwa mambo mengine.
Kulingana na Mkurugenzi wa Shirika lisilo la serikali la IDEA4Africa nchini Rwanda Bi Pamela Munyana, ambao wanaandaa tkuio hilo la wiki ya wajasiriamali,wiki hii inalenga kuwainua wanawake walio na miradi mizuri.
Alisema kwamba wanawake watachaguliwa wikendi hii na kuongeza kuwa shirika lake pamoja na washirika wengine wametafuta pesa za kusaidia miradi ya wanawake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |