Kenya ilikuwa imeruhusiwa kushiriki katika mashindano hayo, baada ya kuondolewa kwa Equitorial Guinea iliyopatikana na kosa la kumchezesha mchezaji wa taifa lingine katika timu yake ya taifa.
Hata hivyo, Equitorial Guinea ilikata rufaa ikisisitiza kuwa mchezaji huyo ni raia wa nchi hiyo , rufaa ambayo imezaa matunda na CAF kukubaliana nayo na kuirejesha timu hiyo kwenye mashindano hayo na kuiondoa Kenya.
Rais wa FKF, Nick Mwendwa, ameiandikia barua na kutaka kuahirisha mashindano hayo au yaendelee lakini yaruhusiwe kuwa na mataifa tisa yatakayoshiriki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |