• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania-Ukosefu wa elimu na mitaji kikwazo kwa wakulima wadogo wa korosho

    (GMT+08:00) 2018-11-12 19:44:47
    Ukosefu wa elimu na mitaji kwa wafanyabiashara wadogo kutoka vikundi vinavyojishughulisha na uzalishaji wa korosho kwa mikoa ya kusini bado ni changamoto katika kufikia malengo ya uchumi wa viwanda.

    Hayo yalibainishwa na katibu wa kikundi cha ujasiriamali cha Amaanan kutoka wilaya ya Newala,Sharafa Mtutuma wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

    Mtutuma alisema kuwa kuna changamoto hiyo kwa wajasiriamali wanaozalisha korosho na kwamba wamejikuta wakikwama,hali ambayo inaweza kukwamisha malengo ya serikali ya kufikia uchumi wa viwanda.

    Katibu huyo alisema kuwa,mbali na changamoto hizo,pia bidhaa mbazo wajasiriamli hao wanazalisha zinaweza zikakosa masoko ya uhakika.

    Kwa upande wake,Naibu Waziri wa Kilimo,Omary Mgumba,aliwataka wajasiriamali wadogo wadogo kuzalisha kwa wingi na kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa ili waweze kujiongezea kipato na kuondokana na umaskini.

    Mgumba alisema kuwa serikali inatambua mchango unaotokana na vikundi vya wajasiriamali wadogo wadogo katika mapambano dhidi ya umaskini,hivyo upo umuhimu wa kuongeza mshikamano katika kuhakikisha kuwa vikundi vinapata mafunzo bora ili kuongeza ufanisi zaidi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako