Katika taarifa waziri wa uchukuzi James Macharia amelitaka shirika hilo kupunguza nauli kwa asilimia 10. Waziri Macharia amesema kuwa hatua hiyo pia itasaidia kufanikisha utekelezaji wa sheria maarufu za Michuki.
Hii leo wananchi wengi wamelazimika kutembea kutokana na mgomo wa magai ya uchukuzi wa umma almaarufu matatu huku wenye magari hayo wakipinga utekelezwaji wa baadhi ya sheria za barabarani maarufu sheria za Michuki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |