Kwa matokeo hayo, Genk inaendelea kuongoza ligi hiyo ikifikisha pointi 35 baada ya kutoka sare mechi 5 kati ya mechi 15 ilizocheza, nyingine zote 10 ikishinda.
Kwa ujumla Samatta amefikisha mechi 129 katika mashindano yote tangu amejiunga na Genk Januari mwaka 2016 akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na amefunga jumla ya mabao 51.
Katika Ligi ya Ubelgiji pekee amefikisha mechi 100 na kufunga mabao 36, Kombe la Ubelgiji mechi nane mabao mawili na Europa League mechi 21 mabao 14.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |