KQ imesema kuwa kutakuwa na ziara moja kila siku kwenda na kutoka Somalia.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari,Mkurugenzi Mkuu wa KQ Sebastian Mikosz alisema ziara hizo zitaanza alhamisi.
Kulingana naye,safari hizo zilianzishwa kutokana na kuongezeka kwa mahitaji katika njia hiyo.
Aliongeza kuwa kuanzishwa kwa safari hiyo kunatarajiwa kukuza biashara katia ya mataifa hayo mawili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |