• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: AFCON U23: Kenya yaichakaza Mauritius, Tanzania yakubali kichapo toka kwa Burundi

    (GMT+08:00) 2018-11-15 08:35:32
    Timu ya taifa ya Kenya ya vijana wenye umri chini ya miaka 23 imeanza vyema kampeni yake ya kusaka tiketi ya kufuzu michuano ya kombe la mataifa ya Afrika (AFCON U23) kwa kuichakaza Mauritius magoli 5-0 katika mchezo mkali uliopigwa ugani Moi Kasarani.

    Nayo timu ya taifa ya vijana ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) imeanza vibaya kusaka tiketi ya kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika (AFCON U23) kwa kukubali kichapo toka kwa Burundi kwa magoli 2-0 mchezo uliopigwa jana mjini Bujumbura.

    Michezo hii ya kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika (AFCON U23) itatumika kwa ajili ya kuwapata wawakilishi wa Afrika katika mashindano ya Olympic yatakayofanyika Japan mwaka 2020.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako