Waziri wa Uhamiaji wa Ugiriki Bw. Dimitris Vitsas ameeleza mpango wa utekelezaji kwa mwaka wa 2019 unaolenga kuboresha hali ya maisha ya wakimbizi ambao bado wamekwama nchini humo. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa kwenye mkutano na waandishi wa habari, wakimbizi na wahamiaji wapatao elfu 42 waliingia Ugiriki kinyume cha sheria mwaka huu. Amesisitiza kuwa serikali ya nchi hiyo itaweka kipaumbele katika kupunguza mzigo kwa vituo vya mapokezi katika visiwa vya Bahari ya Aegean ya Kaskazini ambavyo vimejaa, na kuongeza kasi ya mchakato wa kuwatathimi watu hao wanaotafuta hifadhi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |