• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Iran na Iraq zaahidi kuimarisha uhusiano wao licha ya shinikizo la Marekani

    (GMT+08:00) 2018-11-18 19:27:38
    Iran na Iraq zimetoa mwito wa kuwa na uhusiano wa karibu zaidi licha ya shinikizo jipya la vikwazo kutoka kwa Marekani. Kwenye mkutano na Rais Barham Salih wa Iraq, Kiongozi wa Iran Ayatollah Khamenei amesema Iran iko makini na imedhamiria kuimarisha uhusiano na Iraq.

    Ayatollah amesema Iraq rafiki, yenye nguvu, huru na yenye maendeleo itakuwa na manufaa zaidi kwa Iran, na watu wa Iran watasimama pamoja na wairaq.

    Rais Salih amesema ni fahari kwake kukutana na Ayatollah Khamenei, na kukumbusha kuwa amefanya ziara nchini Iraq kuthibitisha kuwa uhusiano kati ya Iraq na Iran unatokana na historia, na hautabadilika. Amesema Iraq inatarajia kuiga uzoefu wa Iran kwenye ujenzi mpya wa Iraq.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako