Watanzania watafaidika na uwekezaji mkubwa unaotarajiwa kufanywa na makampuni saba ya
Wawakilishi wa makampuni wanatarajiwa kuwekeza katika viwanda vya ujenzi kwa ajili ya uzalishaji wa nguo, sukari, vifaa vya ujenzi na usindikaji wa kilimo.
Akizungumza na mkutano wa waandishi wa habari jana, Naibu waziri wa Mambo ya Nje Damas Ndumbaro alisema wawakilishi wa makampuni watatembelea mikoa ya Dodoma na Simiyu ambapo watashiriki mazungumzo na mamlaka ya serikali katika maeneo husika.
Dkt Ndumbaro amesema Makampuni ya Kituruki yamekuwa yakiwekeza katika mikoa ya Dar es Salaam, Kagera na Mtwara, lakini wakati huu, watawekeza katika makampuni ya nguo katika mikoa ya Dodoma na Simiyu.
Kwa mujibu wa takwimu za biashara za 2017, usawa wa biashara kati ya Tanzania na Uturuki ilikuwa Sh bilioni 8 kwa Tanzania na Sh bilioni 49 kwa Uturuki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |