Fainali hizo zilianza mwishoni mwa wiki iliyopita nchini Ghana, Zambia imepata ushindi mnono wa magoli 5-0 na kuwashangaza Equatorial Guinea ambao walielemewa vibaya.
Matokeo mengine ya kundi B, mabingwa watetezi Nigeria wamelazwa na Afrika Kusini kwa bao 1-0, huku wenyeji Ghana wakiibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Algeria, na Cameroon wakiwashinda Mali mabao 2-1.
Washindi watatu wa kwanza wataliwakilisha bara la Afrika katika fainali za kombe la dunia mwakani jijini Paris Ufaransa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |