Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali shambulizi la kujitoa muhanga lililotokea jana dhidi ya raia waliokusanyika mjini Kabul, Afghanistan kusherehekea siku maalumu ya kidini. Ametoa salamu za pole kwa familia za wahanga na serikali ya Afghanistan, na kutaka juhudi zifanywe ili kuwachukulia hatua za kisheria wahusika wa tukio hili. Watu zaidi ya 43 wameuawa na wengine 83 kujeruhiwa katika shambulizi hilo lililoilenga hoteli moja mjini Kabul. Maimam kadhaa waandamizi wameripotiwa kuwa wahanga.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |