Rais Donald Trump wa Marekani amewasilisha majibu ya maandishi juu ya maswali yaliyotolewa na mchunguzi maalumu Bw. Robert Mueller anayechunguza tuhuma za Russia kuingilia uchaguzi mkuu wa Marekani wa mwaka 2016. Mwanasheria wa rais Trump Bw. Rudy Giuliani ameliambia Shirika la Utangazaji la Marekani ABC kuwa wakati umefika kuuhitimisha uchuguzi huo, ambapo mchunguzi huyo maalumu amepata mashuhuda zaidi ya 30 na kurasa milioni 1.4 za maelezo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |