Kenya inapanga kufungua mkutano wa kwanza wa uchumi wa bahari mjini Nairobi wiki ijayo na kulenga kukuza uchumi kwa kutumia vizuri raslimali ya maji.
Waziri wa mambo ya nje Bibi Monica Juma, amesema mkutano huo wa siku tatu utaifanyia Kenya kuwa kitovu cha ongezeko la uchumi wa bahari linalosaidia kupunguza umaskini, kuongeza nafasi za ajira, kuendeleza viwanda na usimamizi endelevu wa mazingira.
Bibi Juma amesema hivi sasa hatua zimechukuliwa kuhakikisha mkutano huo wa kwanza unafanyika kwa mafanikio.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |