Rais Xi Jinping wa China amerejea Beijing leo mchana baada ya kumaliza ziara yake ya kiserikali nchini Papua New Guinea, Brunei na Philippines.
Katika ziara hiyo, rais Xi alikutana na viongozi wa nchi za visiwa vya Pasifiki, na kuhudhuria mkutano usio rasmi wa 26 wa viongozi wa Jumuiya ya ushirikiano wa kiuchumi ya Asia na Pasifiki, APEC.
Kabla ya kuondoka mjini Manila, rais Xi amekutana na wawakilishi wa Wachina na watu wenye asili ya China nchini Philippines, na kuwahimiza kutoa mchango mpya kwa maendeleo ya Philippines na urafiki na ushirikiano kati ya China na Philippines.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |