Ofisa mwandamizi wa eneo la Meme huko Kumba magharibi kusini mwa Cameroon Bw. Chamberlin Ndong, amesema wanafunzi 9 na mwalimu mmoja waliotekwa nyara Jumanne kwenye shule binafsi huko Kumba wameachiwa huru.
Bw. Ndong amesema wanafunzi hao wameachiwa huru na mwalimu wao aliyejeruhiwa, na wamejumuika na familia zao. Pia amesema wanafunzi hao walitekwa nyara na watu wenye silaha, lakini hawajatangaza sababu ya kuwateka nyara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |