Waziri wa kawi wa Kenya Charles Keter ameliambia bunge la seneti nchini humo kwamba miradi mitatu ya kawi ya mvuke ya megawai 190 haitajiki tena kwani sasa nchi hiyo imeongeza kawi yake kutoka kwa mradi wa kawi ya upepo.
Hata hivyo serikali itahitaji kulipa wamiliki wa miradi hiyo shilingi bilioni 9 ili kuondoa kawi hiyo kutoka kwa gridi ya taifa.
Kandarasi ya kampuni hizo ilipangiwa kukamilika ndani ya miaka 5 ijayo.
Waziri Keter amesema mradi wa kawi ya upepo wa Turkana ambao ulizinduliwa mwezi Oktoba unachangia megawati 240 kwenye gridi ya taifa na hadi sasa Kenya inazalisha megawatt 2,800.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |