Drogba mwenye umri wa miaka 40, anastaafia katika klabu ya Phoenix Rising nchini Marekani.
Alianza kucheza ya kulipwa mwaka 1998 katika klabu ya Le Mans nchini Ufaransa, kabla ya kwenda katika klabu ya Guingamp na baadaye kwenda Marseille.
Hata hivyo, umaarufu wake ulifahamika sana katika klabu ya Chelsea nchini Uingereza, alikofunga mabao 164 katika mechi 341.
Aliichezea timu yake ya taifa kati ya mwaka 2002-2014 na kuichezea mechi 104 na kufunga magoli 65, rekodi ambayo bado anaishikilia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |