Makamu wa rais wa Afrika Kusini Bw. David Mabuza amesema Afrika Kusini itatekeleza mchakato wa mageuzi ya ardhi kwa usimamizi mzuri, wakati watu wa Afrika Kusini wana wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa juhudi za serikali kutaka kutwaa ardhi bila fidia.
Bw. Mabuza amesema hayo wakati akijibu maswali kwenye bunge la Afrika Kusini kuwa mchakato wa mageuzi ya ardhi utakaosimamiwa vizuri, sio tu utaepuka athari mbaya za kutwaa ardhi, bali pia utahamasisha kuingia kwa wadau wapya kwenye sekta ya kilimo bila kuharibu uwezo wa sasa wa uzalishaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |