Sudan na nchi jirani wamesaini azimio la kuongeza usalama wa afya katika eneo la mipakani mjini Khartoum.
Azimio hilo lililosainiwa na Sudan, Chad, Ethiopia, Misri, Libya na Sudan Kusini linalenga kuongeza ushirikiano kwenye sekta ya afya, kutimiza usalama wa afya, kutekeleza kanuni za kimataifa na kuzuia tishio la afya.
Waziri wa afya wa Sudan Bw. Abu Zaid amesema, azimio hilo limeonesha nia ya nchi hizo kukabiliana na changamoto za kiafya. Pia ameongeza kuwa Shrika la Afya Duniani WHO limeahidi kutoa misaada ya fedha na kiufundi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |