Fainali hiyo ya mkondo wa pili imeahirishwa baada ya wachezaji wa Borca Juniors kujeruhiwa vibaya kufuatia basi lao kushambuliwa na vitu vizito na mashabiki wa River Plate.
Shirikisho la soka la Amerika kusini, Conmebol halijaweka wazi mechi hiyo itachezwa lini lakini rais wa shirikisho hilo Alejandro Dominguez amenukuliwa akisema uamuzi wa kuifuta mechi hiyo umetokana na shirikisho hilo kubaini wachezaji wa Boca Juniors bado hawajapona vizuri
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |