Jeshi la majini la Ukraine limesema jeshi la Russia limezifyatulia risasi meli za Ukraine karibu na mlangobahari wa Kerch, na kumjeruhi mtu mmoja na kuharibu meli hizo za kijeshi. Idara ya usalama wa mpaka eneo la Crimea chini ya Shirika la usalama la Russia FSB, imethibitisha tukio hilo na kusema meli tatu za jeshi la majini la Ukraine zilivuka mpaka wa Russia katika Bahari Nyeusi na kufanya vitendo vya hatari kinyume na taratibu za Russia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |