Watu wasiopungua 210 wamejeruhiwa katika tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 6.4 kwenye vipimo cha Richter lililoukumba mji wa Sar Pol Zahab magharibi mwa Iran. Mpaka sasa, hakuna vifo vilivyoripotiwa. Wakati huohuo, shirika la gesi la taifa la Iran limesema mabomba ya gesi katika mji huo yameharibiwa, na limeanza kusambaza nishati kwa waathirika wa tetemeko hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |