Mrithi wa ufalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman bin Abdulaziz amesisitiza kuwepo kwa uhusiano wa kipekee kati ya Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu UAE. Televisheni ya Al Arabiya imesema mrithi huyu wa ufalme alimtumia ujumbe rais Sheikh Khalifa bin Zayed Al Nahyan wa UAE kabla ya kumaliza ziara yake katika nchi hiyo jirani, ikiwa ni kituo cha kwanza cha ziara yake katika nchi za kiarabu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |