• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Kombe la Shirikisho barani Afrika: Wakata miwa wa Turiani Mtibwa waipoteza Northern Dynamo, Kibaya atupia Hat Trick

    (GMT+08:00) 2018-11-28 08:50:48

    Klabu ya Mtibwa Sugar ya Tanzania wameipoteza Northern Dynamo ya Ushelisheli kwa jumla ya mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa Chamazi Complex Dar es salaam kwenye mchezo wa kwanza wa michuano ya shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup).

    Nyota wa mchezo huo alikuwa Jaffary Kibaya wa wakata sukari hao wa Turiani baada ya kupiga Hat Trick na kuondoka na mpira.

    Leo mashabiki wa jijini Dar es salaam watashuhudia mchezo mwingine wa kimataifa ambapo klabu ya Simba ya jijini humo ikiingia uwanja wa taifa kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya klabu bingwa Afrika itakapoikabili Mbabane Swallows ya Eswatini.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako