Meneja wa zamani wa mwenzi wa kimkakati anayeshughulikia masuala ya kimataifa katika mtandao wa kijamii Facebook Bw. Mark Luckie, amesema, Facebook imeshindwa kuwaunga mkono vya kutosha wafanyakazi na watumiaji wake weusi.
Kwenye waraka wa mawasiliano ya ndani uliotolewa wazi jana, Bw. Luckie amesema watu wengi weusi wanajiona kuwekwa pembezoni na kuwa na wasiwasi kuzungumzia uzoefu wao kwenye kampuni hiyo. Pia amesema "watu weusi wanajaribu kuanzisha 'nafasi salama' kwenye Facebook kutokana na kuwa mazungumzo kati yao wenyewe yanaondolewa kwenye jukwaa hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |