Klabu ya Simba ya Dar es salaama Tanzania imeanza vyema michuano ya ligi ya mabingwa Afrika baada ya kuirarua Mbabane Swallows ya Eswatini zamani Swaziland magoli 4-1 katika mchezo wa raundi ya awali ya ligi hiyo uliochezwa jana uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Ushindi huo unamaanisha Simba SC imerahisisha kazi kuelekea mchezo wa marudiano Desemba 4 nchini Swaziland, kwani wenyejii watatakiwa kushinda 3-0 ili kusonga mbele.
Timu nyingine iliyokuwa ikipeperusha bendera ya Afrika Mashariki na Kenya katika michuano hiyo ni Gor Mahia ilipoifunga kwa taabu Nyasa Big Bullets kutoka Malawi kwa goli 1-0 kwenye uwanja wa Moi Kasarani jijini Nairobi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |