• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Ligi ya Mabingwa barani Afrika: Simba na Gor Mahia zaanza vizuri

    (GMT+08:00) 2018-11-29 08:51:09

    Klabu ya Simba ya Dar es salaama Tanzania imeanza vyema michuano ya ligi ya mabingwa Afrika baada ya kuirarua Mbabane Swallows ya Eswatini zamani Swaziland magoli 4-1 katika mchezo wa raundi ya awali ya ligi hiyo uliochezwa jana uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

    Ushindi huo unamaanisha Simba SC imerahisisha kazi kuelekea mchezo wa marudiano Desemba 4 nchini Swaziland, kwani wenyejii watatakiwa kushinda 3-0 ili kusonga mbele.

    Timu nyingine iliyokuwa ikipeperusha bendera ya Afrika Mashariki na Kenya katika michuano hiyo ni Gor Mahia ilipoifunga kwa taabu Nyasa Big Bullets kutoka Malawi kwa goli 1-0 kwenye uwanja wa Moi Kasarani jijini Nairobi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako