Msemaji wa jeshi la Uganda Brigedia Jenerali Richard Karemire amesema, mazungumzo kati ya Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC kuhusu operesheni ya pamoja dhidi ya kundi la uasi la ADF yaliyopangwa kufanyika wikiendi hii, yameahirishwa ili kutoa nafasi ya majadiliano zaidi.
Msemaji huyo amesema, mazungumzo hayo kuhusu operesheni ya pamoja dhidi ya waasi wa ADF ambao hivi karibuni waliwaua walinzi wa amani na askari wa DRC, bado yanapangwa. Tarehe nyingine ya kufanyika kwa mazungumzo hayo itatangazwa baadaye.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |