Mashindano ya taifa ya riadha nchini Tanzania huenda yasifanyike mwaka huu kama ilivyopangwa kutokana na ukata unaolikabili shirikisho la riadha Tanzania (RT).
Akizungumza jana katibu mkuu wa shirikisho hilo Wilhelm Gidabuday amesema shirikisho hilo halina fedha za kuandaa mashindano hayo licha ya kuomba udhamini kwa wafadhili kadhaa.
Kauli ya Gidabuday imekuja siku chache zikiwa zimebaki siku 30 kabla ya mashindano hayo kufanyika. Mbio hizo zimeahirishwa mara mbili kutokana na ukata ambapo kwa mara ya kwanza yalipangwa kufanyika Julai.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |