Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa mataifa UNICEF limesema asilimia 80 ya vijana wanaobalehe wana hatari ya kufa kwa UKIWMI kabla ya mwaka 2030, kama hatua za kuzuia maambukizi hazijaimarishwa.
Taarifa iliyotolewa na shirika hilo kuhusu Watoto, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI inasema kasi ya maambukizi imepungua, lakini kupungua huko hakujawa na kasi ya kuridhisha.
Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, katika mkoa wa kivu Kaskazini kasi ya kupungua kwa maambukizi imeongezeka kutoka asilimia 2.8 ya mwaka jana hadi asilimia 3 ya mwaka huu, ambayo bado si ya kuridhisha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |