Shirika la habari la Sudan SUNA limesema Sudan na Ethiopia zimesisitiza umuhimu wa kuzindua kikosi cha pamoja ili kulinda mpaka wa pamoja.
Pande hizo mbili zimetoa pendekezo hilo kwenye mkutano kati ya msaidizi wa rais wa Sudan Bw. Faisal Hassan Ibrahim na balozi wa Ethiopia nchini humo.
Pande hizo mbili zimekubaliana kuwa uzinduzi wa vikosi vya pamoja utasaidia kuzuia biashara za magendo na usafirishaji haramu wa binadamu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |