Polisi wa Tanzania wamewaua watuhumiwa sita wa ujambazi waliojaribu kumpora mfanyabiashara tajiri. Kamanda wa polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam Bw. Lazaro Mambosasa amesema, watuhumiwa hao walikuwa wanapanga kufanya matukio mbalimbali ya uhalifu.
Kamanda Mambosasa amewakumbusha wananchi wa Tanzania kuwa jeshi la polisi la Tanzania litakuwa makini kuimarisha usalama na maisha na mali za watu, wakati mwisho wa mwaka unakaribia. Amewaonya watanzania wanaotaka kujipatia kipato kwa njia zisizo halali, kuwa hawatakuwa salama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |