Vikosi vya ulinzi wa anga vya Syria vimezuia shambulizi la makombora linaloshukiwa kufanywa na Israel dhidi ya maeneo ya kijeshi kusini mwa Syria. Wakati huohuo shirika la uangalizi wa haki za binadamu la Syria limesema ni Isreal iliyotekeleza shambulizi hilo katika sehemu za kusini na kusini magharibi za viunga vya mji wa Damascus. Israel imekuwa inafanya mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya maeneo ya kijeshi nchini Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |