Ripoti ya Hali ya Chakula ya mwaka 2018 iliyotolewa jana imeonyesha kuwa, tatizo la lishe duni limeendelea kuwa juu na mchakato wa kuondokana na tatizo hilo unazorota, huku eneo la Afrika kusini mwa Sahara likiwa na mzigo mkubwa zaidi.
Ripoti hiyo iliyotolewa jana jijini Nairobi, Kenya imeelekeza kuwa, nchi kadhaa duniani zinakumbwa na aina tatu za lishe duni, ambazo ni watoto kudumaa, upungufu wa damu, na uzito mkubwa. Ripoti hiyo imesema, ingawa katika kiwango cha kimataifa tatizo la watoto walio na chini ya miaka mitano kudumaa linapungua, lakini idadi hiyo inaongezeka barani Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |