• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Xi na Trump wakutana huko Buenos Aires

    (GMT+08:00) 2018-12-02 09:49:39
    Rais Xi Jinping wa China amesema anapenda kubadilishana maoni na rais mwenzake wa Marekani, Donald Trump kuhusu masuala yanayofuatiliwa na pande hizo mbili na uhusiano wa nchi hizo mbili.

    Rais Xi alitoa kauli hiyo katika chakula cha jioni pamoja na rais Trump, akiongeza kuwa anafurahia kukutana na rais Trump.

    Baada ya makutano yaliyopita, rais Xi alisema, hali ya dunia imebadilika sana. China na Marekani zikiwa ni nchi mbili zenye nguvu kubwa za ushawishi zinapaswa kubeba wajibu muhimu katika kuimarisha amani na ustawi duniani, huku ushirikiano ndio ni njia nzuri zaidi.

    Marais hao walikubaliana mwezi uliopita walipoongea kwa simu kwamba wangekutana katika kipindi cha mkutano wa kilele wa kundi la G20, ambapo rais Xi alisema yeye na rais Trump wote wana imani na ushusiano wa China na Marekani pamoja na uhusiano wa kiuchumi na kibiashara.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako