Wajumbe kutoka nchi karibu 200 wameanza majadiliano na kuhimiza kuchukuliwa kwa hatua za haraka kuzuia mabadiliko ya hali ya hewa, miaka mitatu baada ya Makubaliano ya Paris kufikiwa na kuweka lengo la kufanya ongezeko la joto lisizidi nyuzi mbili. Mkutano huo wa wiki mbili unaojulikana kama COP24 unaofanyika mjini Katowice kusini mwa Poland, unalenga kuhitimisha utekelezaji wa miongozo na kuweka bayana utekelezaji wa makubaliano ya Paris kwa njia ya haki kwa nchi zote zilizosaini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |