Maduka ya Carrefour nchini Kenya yamesaini makubaliano ya ushirikiano na kampuni ya kuuza mtandaoni ya Jumia nchini himo.
Kulingana na makubaliano hayo sasa bidhaa za maduka ya Carrefour zitaweza kupatikana kwenye Jumia kuanzia Januari mwaka 2019.
Mkurungezi wa Carrefour nchini Kenya Franck Moreau,amesema makubaliano hayo yatawezesha Carrefour kufikia wateja zaidi hasa wanaopenda kununua mtandaoni.
Aidha matawi ya Carrefourkatika nchi za Afrika Magharibi na kati yamesaini makubaliano kuuza bidhaa kwenye Jumia nchini Ivory Coast, Cameroon na Senegal.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |