Wengi walipitia vichakani na wengine kwenye vichochoro. Waandalizi wa mbio hizo zilizofanyika mjini Shenzhen, wamesema waligundua pia wakimbiaji 18 waliokuwa wamevalia vibango vya nambari za kuwatambua wanariadha vilivyokuwa bandia.
Kulikuwa pia na wanariadha watatu ambao wameelezwa kuwa wanariadha feki waliokuwa wanajifanya kuwa watu tofauti.
Waandalizi wa mashindano hayo wamesema, wanariadha wote waliopatikana wamefanya udanganyifu huo sasa wanakabiliwa na uwezekano wa kupigwa marufuku.
China imeandaa mashindano 1,072 ya marathon na mbio nyingine za nyika mwaka huu, idadi hii ikiwa imeongezeka kutoka 22 mwaka 22, kwa mujibu wa Chama cha Riadha cha China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |