Afrika itakuwa juu kwenye ajenda ya mpango wa kazi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwezi Disemba baada ya Cote d'Ivoire kushika uenyekiti wa zamu wa mwezi huu wa Baraza hilo. Balozi wa Cote d'Ivoire kwenye Umoja wa Mataifa Bw. Leon Adom amesema kutakuwa na mdahalo miongoni mwa wajumbe wa Baraza la Usalama kesho kuhusu ujenzi mpya baada ya mgogoro, utakaohudhuriwa na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guteterres na mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |