Msemaji wa ikulu ya Russia Bw. Dmitry Peskov amesema, nchi hiyo imekubali kufanya tena mkutano wa kilele wa pande nne za suala la Syria utakaohudhuriwa na Russia, Ujerumani, Ufaransa na Uturuki.
Hivi karibuni, rais Vladimir Putin wa nchi hiyo na mwenzake wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan walikutana katika mkutano wa 13 wa kilele wa G20 ambapo walisema, pande hizo mbili zitaendelea kufuata makubaliano yaliyofikiwa awali kuhusu uzinduzi wa eneo lisilo la kijeshi mkoani Idlib, Syria na kuchukua hatua kuhimiza ujenzi wa eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |