Wizara ya Mambo ya Nje ya Ethiopia imewarudisha raia wake 408 kutoka Yemen, na kusema imefanya operesheni hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Uhamiaji la Kimataifa, Shirika la Ndege la Ethiopia na Idara ya Uhamiaji na Masuala ya Kiraia ya Ethiopia. Raia hao wa Ethiopia walikuwa wanatumikia vifungo gerezani kwa kosa la kuingia kiharamu nchini humo. Walitumia Yemen kama kituo cha mpito kuelekea Saudi Arabia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |