• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yaitaka jumuiya ya kimataifa izihimize nchi zilizoendelea kutekeleza ahadi za kutoa msaada wa maendeleo

    (GMT+08:00) 2018-12-05 17:57:37

    Balozi wa kudumu wa China kwenye Umoja wa Mataifa Bw. Ma Zhaoxu amesema, jumuiya ya kimataifa inapaswa kuzihimiza nchi zilizoendelea kutekeleza ahadi za kutoa msaada wa maendeleo, na kuweka mazingira ya kimataifa yanayosaidia maendeleo ya nchi zinazoendelea zikiwemo zile zenye kipato cha kati.

    Balozi Ma amesema, hivi sasa nchi nyingi zinazoendelea zinakabiliwa na changamoto za maendeleo, jumuiya ya kimataifa inapaswa kuzingatia kwa pande zote kiwango cha maendeleo cha nchi zenye kipato cha kati, kuimarisha uhusiano wa wenzi duniani, na kujenga mfumo wa ushirikiano unaoongozwa na Umoja wa Mataifa, kuuchukua ushirikiano kati ya Kaskazini na Kusini kuwa njia muhimu huku ukichukua ule kati ya Kusini na Kusini kama njia ya kuusaidia, ili kuunga mkono maendeleo ya nchi zinazoendelea.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako