Kampuni ya mawasiliano ya Bharti Airtel Afrika Mashariki imepata dola milioni 473 katika kipindi kilichokamilika mwezi Septemba.
Kampuni hiyo imesema mapato hayo ni ya ununuzi wa data za intaneti.
Kipindi sawa na hicho mwaka jana mapato ya mauzo ya data yalifikia dola milioni 212.
Nayo mapato ya huduma ya kupiga simu nchini Kenya, Tanzania, Uganda na Rwandan yaliongezeka kwa asilimia 6.2 hadi dola milioni 169 ikilinganishwa na dola milioni 159 za mwaka jana.
Wakati huo huo kampuni hiyo imechaua benki za Goldman Sachs na J.P. Morgan kusimamia mauzo yake ya kwanza ya hisa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |