Kampuni ya kuzalisha kawi nchini Kenya Kengen, imeanza ujenzi wa mradi wa kuzalisha megawati 83 za kawi ya mvuke katika eneo la Naivasha.
Ujenzi wa mradi huo uliozinduliwa na Rais Uhuru Kenyatta unatarajiwa kukamilika mwaka 2021.
Kengen inapanga kuongeza megawati 720 za kawi endelefu.
Hadi sasa Kengen imezalisha megawati 1,631miradi mingi yake ikiwa ni kawi ya maji.
Pamoja na makampuni ya kibinafsi sasa Kenya ina kawi ya megawati 2,370.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |